DONDOO ZA MAISHA YA KILA SIKU

May 2020

                               


MAHUSIANO YAKO YANACHANGIA MAFANIKIO YAKO.
Mahusiano  ni muhimu sana kwa maisha yetu, mahusiano yanauwezo wa kukujenga  au kukupoteza kabisa mahusiano mengi ya kwetu hua yanatuonyesha  na kutuinua kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Ni muhimu  sana  kua na mahusiano  ambayo yanatujenga na kutusogeza, kua na watu watu ambao wanaona ile ndoto iliyoko ndani yako, watu  wanaofahamu unafanya nini na  wanakusupport  kwa  kila hatua  unayopiga, kukuamsha kila siku Asubuhi na kukumbusha kufanyia kazi ndoto zako.
     Tunahitaji marafiki ambao wanafahamu kitu gani ni bora kwako na ndoto  zako ni zipi na wakati mwingine kukupa ata mwangaza na njia za wewe kufika hapo ulipo, marafiki ambao unaweza kuamka asubuhi au  usiku wa manane  watapokea simu na kusikilza shida yako na kama kuna namna  ya kukusaidia watafanya ivyo bila kuomba samahani/Hudhuru  kwa kutokufanya yale ambayo unayotaka wakusaidie
                          AINA YA MARAFIKI WANAOJENGA.

  • RAFIKI AMBAE ANA MTAZAMO CHANYA.

Tuna marafiki  wengi  sana na mitazamo yetu na yao ni muhimu kufanana ili kuweza  kufanya kazi au kuendana katika mambo mengi,tunahitaji watu  ambao watu  wanamitazamo  chanya kwenye kila kitu na watu ambao wana mbinu mbadala  kila wakati  ili kutukomboa kwa kila hali tunazokutana nazo kila wakati.Kufahamu na kuambiwa shida haitakiwi kukaa  na kua na matazamo hasi katika  hilo tatizo ila kua chanya na kua na mbinu ya kulikabili hilo tatizo wakati linapokuja na sio tu katika tatizo hata mipango yako atakua mstari wa mbele kukushawishi kujaribu maana anaelewa

  •     RAFIKI MKWELI.

Ukweli humfanya mtu kua huru   pamoja na kwamba ukweli ni mchungu  na mara nyingi hauonekani kama ni mzuri kwetu lakini tunauuhitaji na  ukweli na kuna  wakati ni mzito lakini hutusaidia kufika kwenye sehemu tunayohitaji  Kufika na rafiki Mkweli hukufanya wewe kujifahamu na   kufikia Malengo yako maana utafahamu  sehemu gani unahitaji marekebisho sehemu gani unahitaji kubadilika na sehemu gani uongeze juhudi zaidi, Sisi hatujioni   na hatuwezi tukajisemea  na kufanya vitu  vyetu lakini tunahitaji marafiki ambao watatushika mkono na kutueleza ukweli  bila kujali wanatuumiza lakini pia kwa kuokoa nafsi zetu na malengo yetu.

  •     RAFIKI MWENYE KUFARIJI/KUTIA MOYO.

  Tunapigana  sana   katika maisha  na tunaaguka mara nyingi  na tunahitaji watu  wa kutuinua  tena sio kwa kutupa fedha wala magari bali  kutufariji na kufanya mioyo yetu kupiga  tena ,Rafiki mwenye kutia moyo ni mali na  thamani  na anapaswa kulindwa,Tunafahamu kua pengine na yeye ana mambo yake  mengi tu lakini kuamua kukusikiliza na kukufariji ni zawadi kubwa sana  zaidi ya kukupa gari au fedha,Usimwache rafiki wa namna hii maana uyu ndie atakusuport katika kitu chako kwa maana furaha yako ni yake na hayupo tayari kuipoteza kwa namna yoyote ile.
   Mithali 27;9,19
Marhamu na manukato  hufurahisha moyo,Kadhalika utamu  wa rafiki ya mtu  utokao katika kusudi la moyo wa mtu.
19;Kama ufananavyo  na uso katika maji ;Kadhalika  moyo wa mtu na mwenzake.
   

Comments

Popular Posts

ZANA ZA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA

NUKUU ZA SOMO LA TEHAMA MWAKA WA PILI MEI 2020

Maswali ya TEHAMA ngazi ya certificate