. Ni mambo gani muhimu hufanyika katika vyuo vya Ualimu daraja “A” yanayohusika na kumwandaa mwalimu tarajali wa shule za msingi? Hufundishwa masomo ya saikolojia, falsafa ya Elimu, Misingi ya Elimu, Mitaala na ufundishaji na Njia mbalimbali za kufundisha masomo; Hujifunza kuandaa maazimio ya kazi na maandalio ya somo; Hujifunza taratibu, sharia na miiko ya kazi, Hufanya mazoezi ya kufundisha. 2. Kwa nini saikolojia ni taaluma ya sayansi? Kwa ujumla saikolojia ni taaluma ya kujifunza tabia na mwenendo wa viumbe, ni taaluma ya kisayansi kwa kuwa huhusika na kujifunza na kupambanua kwa undani mabadiliko ya tabia ya binadamu kutokana na kubadilika kwa vipindi vya ukuaji kwa kiumbe na mazingira anamoishi. 3. Saikolojia ya mtoto ni nini? Saikolojia ya mtoto ni tawi la elimu linaloshughulikia taaluma ya kujifunza tabia na mwenendo wa mtoto katika hatua mbalimbali za ukuaji wake. 4. Mabadiliko gani yanatokea kwa mtoto kati ya umri wa miaka 2 – 5? Hiki kinaitwa kipindi cha utoto kwani; Mi...
Comments
Post a Comment